FAHAMU KWA HARAKA: DeFi NI NINI?

Leo tujifunze DeFi (Decentralized Finance) - hii ni moja ya nguzo muhimu sana kwenye crypto na blockchain.

DeFi ni nini?

DeFi ni kifupi cha Decentralized Finance, yaani huduma za kifedha zisizo na benki au mtu wa kati, zinazoendeshwa na blockchain, hasa Ethereum.

Kwa lugha nyepesi: DeFi ni benki ya mtandaoni isiyo na benki,

πŸ‘‰ Hakuna manager, hakuna karani, hakuna makaratasi,

πŸ‘‰ Wewe na blockchain mnafanya miamala moja kwa moja.

Kupitia DeFi unaweza:

1.Kukopesha pesa (crypto)

2.Kukopa pesa

3.Kupata riba

4.Kufanya trading

5.Kuweka akiba

6.Kununua insurance

7.Kuweka bets (long & short)

Yote haya bila benki.

Kwa nini DeFi ni muhimu?πŸ‘‡

Bitcoin ilianza kama pesa ya kidigitali

DeFi ikaenda mbali zaidi:

πŸ‘‰ Ikajenga mfumo mzima wa kifedha mbadala wa Wall Street,

πŸ‘‰ Bila majengo makubwa,

πŸ‘‰ Bila mishahara ya mabenki,

πŸ‘‰ Bila vikwazo vya nani aruhusiwe au asiruhusiwe.

Mtu yeyote mwenye Simu, Internet,Wallet anaweza kushiriki DeFi

Hii ina maana kuwa:

- Fursa sawa kwa wote

- Hakuna kubaguliwa

- Hakuna kuulizwa β€œunafanya kazi gani?”

Faida za DeFi

_1. Iko wazi kwa wote_

Huhitaji kufungua akaunti benki. Unatengeneza wallet tu kama MetaMask then unaanza.

_2. Hakuna taarifa binafsi_

Hakuna jina

Hakuna email

Hakuna NIDA

Hakuna KYC

Wallet yako ndio utambulisho wako.

_3. Uhuru kamili_

Unaweza kutuma pesa muda wowote

Hakuna kuomba ruhusa

Hakuna kusubiri siku 3-5

Hakuna ada kubwa za kibenki

5. _iko chapu sana_

Riba hubadilika kila sekunde chache (kama sekunde 15)

Mara nyingi riba ni kubwa kuliko benki za kawaida

_6.Transparent_

Miamala yote iko wazi kwenye blockchain

Kila mtu anaweza kuona kilichofanyika

Hakuna kuficha hesabu kama kampuni binafsi

DeFi inafanyaje kazi?

Badala ya benki, DeFi hutumia DApps (Decentralized Applications).

DApps ni apps zinazotengenezwa juu ya blockchain hasa Ethereum

Mfano

Unafungua DApp

Unaconnect wallet yako

Unaanza kutumia huduma

Hakuna fomu, Interview wala Approval ya mtu

Matumizi ya DeFi kwa sasa

1. Kukopesha

Unakopesha crypto yako,

Unapata riba kila dakika, sio mwisho wa mwezi.

2. Kukopa pesa

Unakopa papo hapo

Hakuna makaratasi

Kuna hadi flash loans (mikopo ya sekunde chache)

Benki za kawaida haziwezi hili.

3. Trading

Unanunua na kuuza crypto moja kwa moja

Hakuna broker

Hakuna middleman

Ni kama trading ya hisa bila broker.

4. Akiba

Unaweka crypto kwenye platforms za DeFi, Unapata riba nzuri kuliko benki nyingi.

5. Derivatives (Long & Short)

Unabet bei ipande (long)

Unabet bei ishuke (short)

Ni kama options au futures kwenye soko la kawaida.

Hasara na hatari za DeFi

Tusifundishe DeFi bila kuongelea hatari

1. Ada za mtandao (Gas fees)

Ethereum chain ikizidi kuwa busy, ada inapanda

Hivyo ku trade mara nyingi inaweza kuwa ghali

2. Volatility

Bei hubadilika haraka

Unaweza kupata faida au hasara kubwa

3. Kodi na sheria

Hakuna mtu anayekufanyia hesabu za kodi

Wewe mwenyewe unatakiwa kufuatilia

Sheria zinatofautiana nchi hadi nchi

Hitimisho

DeFi ni: - Mfumo wa kifedha wa kizazi kipya

- Usio na benki

- Wazi kwa wote

Lakini una hatari zake

πŸ‘‰ Elimu ni muhimu kabla ya kutumia DeFi.

Reply to this note

Please Login to reply.

Discussion

No replies yet.